Pages

Monday, February 8, 2016

Mapishi ya Jamii ya Tambi na Mayai


Mahitaji
  • Tambi
  • Mayai
  • Nyanya
  • Vitunguu
  • Karoti
  • Hoho
  • Mdalasini uliosagwa
  • Mafuta ya kupikia 
  • Maji


Jinsi ya kuandaa na kupika
  • Katakata tambi zako kwa urefu unaoutaka kisha ziloweke kwenye maji safi ya baridi hadi zilainike.
  • Katakata viungo vyote  ( Vitunguu, Nyanya, Hoho, Karoti) kisha weka kwenye sahani safi.
  • Gonga Mayai yako yanayotosha idadi ya Tambi na kisha weka kwenye bakuli.
  • Weka sufuria jikoni na uweke mafuta hadi yachemke.
  • Chukua Tambi zilizolowekwa kwenye maji na uziweke jikoni kwenye mafuta yanayochemka huku ukizigeuza geuza hadi zitapoonyesha dalili ya kuiva.
  • Changanya mchanganyiko wa Mdalisi kwenye Tambi.
  • Changanya mchanganyiko wa viungo huku ukiendelea kugeuzageuza hadi viungo viive.
  • Funika mchanganyiko wako na uuache uive  hadi utapohakikisha maji yamekauka.
  • Baada ya kujiridhisha kuwa chakula chako kimeiva kiipue .
  • Weka Mayai yaliyopasuliwa kwenye chakula chako na ugeuze hadi mayai yatapoiva na mvuke.
  • Chakula chako kupi tayari kwa kuliwa.


Maelezo zaidi
Chakula hiki kinaweza kuliwa na watu wa rika zote na unaweza kutumia juice katika mlo huu.

0 comments:

Post a Comment